NOTE! This site uses cookies and similar technologies.

If you not change browser settings, you agree to it.

I understand

Reporting the underreported about the plan of action for People, Planet and Prosperity, and efforts to make the promise of the SDGs a reality.
A project of the Non-profit International Press Syndicate Group with IDN as the Flagship Agency in partnership with Soka Gakkai International in consultative status with ECOSOC.


SGI Soka Gakkai International

 

Picha: Picha ya kiwamba ya Mkutano wa mtandaoni wa EEPA mnamo Mei 25.

Na Reinhard Jacobsen

BRUSSELS (IDN) — Kiwango na ukatili wa uhalifu wa unyanyasaji wa kingono unaohusiana na mizozo dhidi ya wanawake uliofanywa huko Tigray umesababisha kushutumiwa kote ulimwenguni.

Haikushangaza kwamba Mpango wa Nje wa Ulaya na Afrika (EEPA) ulizingatia mada hiyo katika Mkutano wa mtandaoni ulioandaliwa mnamo Mei 25. EEPA ni kituo cha utaalam kilichoko Ubelgiji na maarifa ya kina, machapisho, na mitandao, iliyobobea katika maswala ya ujenzi wa amani, ulinzi wa wakimbizi, na uthabiti katika Pembe ya Afrika.

Image credit: UNCCDC

Na Rita Joshi

BONN (IDN) – Mpango wa Ukuta Mkubwa wa Kijani (GGW) kwa zaidi ya karibu miaka 13 umerejesha karibu hekta milioni 20 za ardhi, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa Septemba tarehe 7 katika mkutano usio bayana wa mawaziri wa mazingira kutoka Senegali, Mauritania, Mali, Bukina Faso, Naija, Naijeria, Chadi, Sudani, Eritrea, Uhabeshi na Jibuti pamoja na washirika wa kikanda, mashirika ya kimataifa na mashirika ya maendeleo.

Mpango wa GGW ulizinduliwa mnamo mwaka wa 2007 chini ya uongozi wa Tume ya Umoja wa Afrika na Shirika la Muungano wa Afrika, na kwa msaada wa kifedha kutoka kwa serikali ya Ayalandi.

Photo: With the lockdown to fend off the spread of COVID-19, many Southern Africans, have lost their jobs and switched to vending on the streets where they engage in cat and mouse games with police enforcing lockdown rules. Consequently, the game to survive still remains tough for most Africans as they battle to support their children amid schools closure. Credit: Jeffrey Moyo | INPS-IDN

Na Jeffrey Moyo

MUSINA, Afrika Kusini (IDN) – Watoto wake watatu wa ujana hucheza mpira wa karatasi uliotengenezwa nyumbani kwenye barabara zenye vumbi za Musina, vitabu vya kuandika vimetawanyika kwenye varanda ya nyumba yao ya kukodi katika mji wa mpakani mwa Afrika Kusini na Zimbabwe. Walakini Gerald Gava, baba wa watoto mwenye umri wa miaka 47, hulala kwenye mkeka uliotandazwa kwenye varanda, inavyoonekana hana chochote cha kufanya baada ya kuacha kufanya kazi miezi mitatu iliyopita wakati kuzuiliwa kuliathiri kampuni ya ujenzi iliyomuajiri.

Photo: Women tend a community nursery created as part of a completed ITTO project to assist forest landscape restoration in Togo. Credit: ODEF

Na Ramesh Jaura

BERLIN | TOKYO (IDN) – Togo iliyoko Afrika Magharibi ni mahali pa mradi wa hatua muhimu kati ya Soka Gakkai, shirika la jamii ya kimataifa ya Wabudha na Shirika la Kimataifa la Mbao za Kitropiki (ITTO). Mashirika hayo mawili yametia saini memoranda ya kuzindua mradi wa upanzi wa miti unaotoa fursa za mapato kwa vikundi vya wanawake katika maeneo mawili ya vijijini nchini Togo.

Memoranda inayohusisha mchango wa yen milioni 10 (Dola za Marekani 93,300) kwa awamu ya kwanza ya mwaka mmoja ya mradi huo ilisainiwa mnamo Julai tarehe 1 katika makao makuu ya Soka Gakkai (SG) huko Tokyo. Mradi utaanza Septemba tarehe 1.

Picha: Abiria anaosha mikono kwa kutumia kifaa kipya kabla ya kuabiri gari la huduma ya umma katika Kituo cha Mabasi cha Uwanja wa Soko la Mungatsi, Kaunti ya Busia, Kenya. Hisani: Kevin Wafula.

Na Justus Wanzala

BUSIA, Kenya (IDN) – Ni mchana wenye joto katika kituo cha mabasi katika kituo cha soko cha Mungatsi, Kaunti ndogo ya Nambale, katika Kaunti ya Busia, Magharibi mwa Kenya. Watu wengi, idadi kubwa yao wasafiri wanapanga foleni kuosha mikono yao. Kila mtu anadumisha umbali kutoka kwa mwingine wakati wanaosha mikono yao na kuabiri magari ya huduma za umma wakielekea maeneo yao mbalimbali.

Kuenea kwa virusi vya korona kuliathiri Afrika na video iliyohuishwa na INPS-IDN.

Na Lisa Vives, Mtandao wa Taarifa wa Kimataifa

NEW YORK (IDN) – Wakati Afrika, kama jamii ya kimataifa kwa ujumla, inashiriki katika vita vikali dhidi ya virusi vya korona, mtaalamu wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) ameuliza kuhusu makadirio ya kutisha ya wale walioathiriwa na COVID-19. Wakati huo huo, Ghana kwa hatua ya mshangao imeamuru kuondolewa kwa kusitishwa kwa shughuli za kawaida kwa kiasi fulani. Kirusi kilichoenea sana kinaingiza Rwanda katika 'mikopo' mikubwa chini ya upunguzaji wa deni.

Picha: Picha ya wanachama wa jamii wa Pardhi, Maharashtra, India (Juni 7, 2019). Hisani: UNICEF | Sri Kolari

Na Jaya Ramachandran

NEW YORK (IDN) – Ikilinganishwa na bilioni 7.7 leo, karibu watu bilioni 8.5 wanatarajiwa kukaa katika sayari ya Dunia kwa muda mfupi zaidi ya miaka kumi, na karibu bilioni 10 ifikapo mwaka wa 2050, na nchi chache tu zenye ongezeko kubwa, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa.

Matarajio ya Idadi ya Watu 2019: Mambo muhimu, yaliyochapishwa na Idara ya Idadi ya Watu wa Idara ya Umoja wa Mataifa ya Mambo ya Uchumi na Kijamii (UN DESA), yanatoa maelezo ya kina ya mifumo ya kimataifa ya idadi ya watu na matarajio. Utafiti unahitimisha kwamba idadi ya watu duniani inaweza kufikia kilele chake ikikaribia mwisho wa karne ya sasa, kwa kiwango cha karibu bilioni 11.

Picha: Wanawake wanashiriki katika maandamano kupinga ulipizaji wa kingono huko Dar es Salaam mwaka wa 2018. Hisani: Edwin Mjwahuzi

Na Kizito Makoye

DAR ES SALAAM (IDN) – Bango lenye ujumbe "Hitimu na ‘A’ sio na UKIMWI" katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, linaeleza hadithi mbaya ya wanafunzi wa kike ambao hushiriki ngono ili kupata alama za juu.

"Mwalimu wangu alitaka kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mimi. Nilipokataa matakwa yake ya ngono, alilipiza kisasi kwa kunipa alama za chini," anasema Helena (si jina lake halisi).

Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 23 anayesomea sheria, ambaye amepitia utendaji duni katika masomo yake, anazidi kuwa na wasiwasi kuhusu hatma yake ya kitaaluma.

Page 2 of 4

Newsletter

Striving

Striving for People Planet and Peace 2022

Mapting

MAPTING

Partners

SDG Media Compact


Please publish modules in offcanvas position.