Na Rita Joshi
BONN (IDN) – Mpango wa Ukuta Mkubwa wa Kijani (GGW) kwa zaidi ya karibu miaka 13 umerejesha karibu hekta milioni 20 za ardhi, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa Septemba tarehe 7 katika mkutano usio bayana wa mawaziri wa mazingira kutoka Senegali, Mauritania, Mali, Bukina Faso, Naija, Naijeria, Chadi, Sudani, Eritrea, Uhabeshi na Jibuti pamoja na washirika wa kikanda, mashirika ya kimataifa na mashirika ya maendeleo.
Mpango wa GGW ulizinduliwa mnamo mwaka wa 2007 chini ya uongozi wa Tume ya Umoja wa Afrika na Shirika la Muungano wa Afrika, na kwa msaada wa kifedha kutoka kwa serikali ya Ayalandi.